Jumapili, 22 Novemba 2015

EGG KEBAB(JICHO LA MKE MWENZA)


MAHITAJI
1.Nyama ya kusaga robo
2.Mayai 10
3.Kitunguu maji kikubwa 1
4.Kitunguu thomu punje 5
5.Mdalasini wa unga nusu kijiko cha chakula
6.Uzile(Binzari nyembamba) kijiko 1 cha chakula
7.Pilipili manga nusu kijiko cha chakula
8.Pilipili ya kuwasha 1
9.Chumvi kiasi
10.Mafuta ya kupikia nusu lita
11.Karoti 1
12.Pilipili boga(Pilipili hoho) 1
13.Paprika(sio lazima) nusu kijiko cha chakula

MAANDALIZI
1.Osha vitu vyako vyote vinavyo hitajika kuoshwa
2.Katakata vitunguu maji vidogo vidogo kwa umbo la pembe nne(Square)
3.Para keroti yako kwa kutumia Grater(Kipario)
4.Katakata Pilipili hoho kwa umbo la pembe nne(Square)
5.Twanga kitunguu thomu,chumvi na ndimu
6.Vunja Mayai 3 weka chumvi na uyapige pige na umma

JINSI YA KUPIKA
1.Chemsha mayai 7 na chumvi mpaka yaive
2.Chemsha nyama ya kusaga na chumvi na ndimu
3.Weka karoti,pilipili hoho,kitunguu maji,pilipili uloitwanga,viungo vya unga changanya vizuri
4.Menya Mayai yako kisha yakate kati sehemu mbili sawa
5.Toa viini viweke kwenye nyama ya kusaga na uichanganye vizuri
6.Tengeza nyama yako shape ya duara 
7.Weka vile viduara vya nyama kati kati ya yai ulolipasua
8.Weka mafuta jikoni yaache yapate moto
9.Chovya egg kebab zako kwenye mayai mabichi na chovya kwenye karai la mafuta
10.Ziache kwa dakika 3 kisha zigeuze
11.Baada ya dakika 2 zitoe ziweke kwenye chujio au tissue
12.Acha zipoe tayari kwa kula
NB:1.Hakikisha mayai yanaiva vizuri
      2.Hakikisha mafuta yanapata moto vizuri kabla kuzichovya ili yai na nyama zisiachane

Furahia Egg Kebab Zako.

0 comments:

Chapisha Maoni