Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Ramadhan Recipe. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Ramadhan Recipe. Onyesha machapisho yote

Ijumaa, 10 Juni 2016

MUHOGO WA NAZI(CASSAVA WITH COCONUT MILK SAUCE)


MAHITAJI/INGREDIENTS
1.Muhogo kiasi(kama mitano)
2.Nazi ndogo iliokunwa
3.Nyanya(Tungule) ndogo 2
4.Kitunguu maji kidogo 1
5.Pilipili Hoho(Pilipili boga) 1
6.Keroti 1
7.Pilipiil Mbuzi 1
8.Nyanya ya paket(Tomato paste) kijiko 1
9.Ndimu ndogo 1
10.Chumvi kiasi
11.Maji kiasi
12.Fish Masala kijiko cha chai 1
13.Kitunguu thomu kilotwangwa kijiko cha chai 1
14.Samaki kiasi upendacho


MAANDALIZI/PREPARATION
1.Menya muhogo kata kata vipande vidogo vidogo
2.Ioshe kwa maji safi
3.Weka kwenye sufuria na maji kiasi
4.Weka maji kwenye nazi iliokunwa
5.Chuja tui zito la kwanza
6.Kisha chuja tui la pili jepesi ujazo wa vikombe 3 vidogo vya chai au zaidi
7.Osha viungo vilobakia
8.Katakata vyote kwa pamoja(Kitunguu maji,keroti na pilipili hoho,nyanya)
9.Osha samaki weka kwenye sufuria



JINSI YA KUPIKA/HOW TO COOK
1.Weka chumvi kwenye sufuria ya muhogo
2.Weka jikoni acha uchemke mpaka uive na kuwa laini
3.Kamua ndimu na maji kidogo kisha mimina kwenye sufuria yenye samaki
4.Weka fish masala kwenye samaki
5.Iweke jikoni funika kwa dakika moja acha samaki aive kidogo kwa mvuke
6.Malizia kuweka viungo ulivyo vikatakata katika hatua namba 8 pamoja na pilipili
7.Weka nyanya ya paket kisha funika kidogo wacha viive hakikisha samaki hakauki na kuwa mkavu
8.Muhogo ukiiva mwaga maji yote bakisha muhogo mkavu
9.Mimina tui la pili lile jepesi kwenye muhogo
10.Ongeza na chumvi rudisha muhogo jikoni
11.Acha uchemke mpaka tui lipungue kidogo mimina tui la pili
12.Baada ya dakika moja mimina samaki mwenye viungo kwenye muhogo wako
13.Acha kwa dakika 1 nyengine epua
14.Acha upoe kisha toa samaki weka pembeni
15.Chukua mwiko uchanganye vizuri muhogo uchanganyike na vile viungo
16.Pakua sahanini na muweke samaki wako juu ya muhogo tayari kwa kula

Angalizo:Note
1.Hakikisha unatafuta muhogo ambao sio mchungu
2.Usichemshe muhogo mpaka ukaiva sana pia usiuwahishe ukawa haujaiva
3.Tui la pili ukiweka lifunike muhogo kidogo
4.Ukisha kuweka tui la pili usiuache muhogo ukakauka ukakosa rojo rojo

Furahia Muhogo wako.

Ijumaa, 25 Desemba 2015

CHAPATI ZA MAJI(PANCAKES)


MAHITAJI/INGREDIENTS

1.Unga wa ngano nusu kilo
 1/2 kilogram of All Purpose flour

2.Kitunguu maji kikubwa 1
 1 big Onion

3.Pilipili boga 1
 1 Green pepper

4.Karoti 1
 1 Carrot

5.Yai 1
 1 Egg

6.Chumvi cha chakula 1
 1 Tbsp of Salt

7.Mafuta nusu kikombe
 1/2 cup of Cooking oil

8.Maji kikombe kikubwa 1 au zaidi
 1 Big Cup of water or more

9.Sukari kijiko cha chai kimoja 1
 1/2 Tbsp of sugar


MAANDALIZI/PREPARATION
1.Chukua bakuli kubwa kiasi chekecha unga weka pembeni
 Sift the flour in a big bowl and keep it a side.

2.Kata kata vitunguu maji kama vya mchuzi vifikiche kwa mkono kuviachanisha weka pembeni
 Cut the onion in small sized pieces and crumble them by your hand

3.Para karoti weka pembeni
 Grate the carrots

4.Kata pilipili boga nyembamba weka pembeni
 Cut thin and small pieces of  green pepper

5.Vunja yai kwenye kibakuli lipige na umma kama unataka kulikaanga weka pembeni
 Take a small bowl and folk then beat an egg keep it a side

6.Chukua maji weka kidogo kidogo kwenye unga huku ukiuchanganya na mchapo au upawa mpaka uwe na uzito kiasi hakikisha hauwi mwepesi sana wala mzito sana
 Pour water slowly in a flour and mix it well then whisk the wet mixture and make it neither heavy nor light

7.Mimina vitunguu,karoti na pilipili boga kisha koroga uchanganye vizuri
Put onion,carrots and green pepper in your wet mixture and whisk it 

8.Weka chumvi ,sukari na yai kisha changanya vizuri mpaka uji wako uchanganyike na vitu vyote
 Put salt,sugar and bitten egg and keep whisk the mixture till all ingredient well mixed

JINSI YA KUPIKA/HOW TO COOK
1.Weka chuma(frying pan) chako jikoni na mafuta kijiko kimoja yaeneze kwenye chuma chote
 Pour a Tbsp of oil in Non Stick Frying Pan and swirl around so that it lightly coats the surface,let it heated for a minute

2.Tumia upawa chota miko miwili au zaidi inategemea na ukubwa wa chuma chako na ieneze kwenye chuma chote
Use a cooking spoon mix well your wet mixture then take two of them and pour the mixture in a frying pan

3.Acha kwa dakika 3 mpaka uone mkate wote umekauka ile umaji maji wa ubichi haupo
  Let cooked for 3 minutes till the upper side become dry

4.Ugeuze upande wa pili uache pia kwa dakika 3 ukauke
 Carefully lift the edge of the pancake with spatula and flip on the another side and cook again till dried for about 3 minutes

5.Chota mafuta kijiko kimoja weka chini ya mkate wako huku ukiuzungusha mpaka upate yangi ya kuvutia
 Put a Tbsp of oil at bottom of your cooked pancake and use a Tbsp to squeeze it till have golden brown colour

6.Ugeuze kisha utoe weka kwenye kwenye sahani
 Flip over and and remove it from pan to the plate

7.Rudia njia hizi mpaka umalize uji wote
Repeat the above procedure till you finish the whole wet mixture

8.Weka mezani kula na chai ya maziwa,juice au kinywaji chochote
 Serve with tea,milk,juice or any drink

Angalizo:Note
1.Yai muhimu usipoweka mikate inaganda kwenye chuma
 You must put an egg otherwise the pancake will sticky in pan 

2.Kama utakosa yai weka mafuta kijiko 1 cha chakula
 Use a Tbsp of cooking oil in absence of an egg

3.Tumia Nonstick Frying Pan kwa kuhofia kugandisha mikate mara kwa mara
 Use Nonstick Frying pan to avoid sticking of pancakes frequently

4.Ili upate mikate mizuri ya kuvutia hakikisha moto ni wa wastani ukipikia moto mkubwa zinakua mbaya
 Use medium heat to get delicious and attractive pancakes otherwisewont have good taste

Furahia Chapati Zako.

Jumanne, 22 Desemba 2015

NDIZI MBIVU(HOW TO COOK PLANTAIN WITH COCONUT MILK)



MAHITAJI/INGREDIENTS
1.Ndizi mbivu(Mkono wa tembo) 4
 4 Plantains 

2.Nazi kubwa 1
 1 Large Fresh Coconut

3.Sukari kikombe kidogo 1
 1 Small Cup Sugar

4.Arki Vanilla kijiko cha chai 1
 1 Tea Spoon Vanilla 

5.Chumvi kiduchu
 Pinch of Salt

6.Hiliki punje 10
  10 Cloves of Cardamom 

7.Zabibu pakti Ndogo 1
 1 Small Packet Raisins 
8.Custard kijiko cha chakula 2
  2 Tbsp Custard Powder
  
9.Maji kiasi
  Some Water 

MAANDALIZI/PREPARATIONS
1.Osha ndizi zikiwa na maganda yake vizuri
  Wash the plantains with clean water
2.Kata ndizi yako sehemu mbili sawa upate vipande viwili
  Cut the plantains into halves

3.Pasua ndizi katikati kisha imenye maganda usiyatupe yaweke pembeni sehemu safi
  Slice one half at the center ,remove the skin and keep them aside for other uses

4.Weka maganda yako kwenye sufuria unayopikia yapange vizuri
  Place the skin in the pan that you will use for cooking the plantains

5.Weka ndizi juu ya maganda yake zipange vizuri kwenye sufuria
   Add the peeled plantains on top of  skin

6.Kuna nazi kisha saga kwenye blenda au chuja kwa mkono
   Grate the coconut and blend it or use your hand to get coconut milk

7.Weka tui zito mbali na tui jepesi mbali
   Make sure you separate the heavy coconut milk and light one

8.Twanga hiliki mpaka iwe ya unga
  Grind the cardamom seeds to get cardamom powder

JINSI YA KUPIKA/HOW TO COOK
1.Chukua tui jepesi na chumvi mimina kwenye sufuria ya ndizi
  Pour light coconut milk in the pan contained plantains ,add salt too

2.Kisha weka sukari na zabibu weka jikoni zifunike ziache kwa dakika 10 zikichemka
  Add sugar and raisins,then cover the pan let it cooked for 10 minutes

3.Baada ya dakika hizo weka arki, hiliki na tui zito ila libakishe kidogo
  Add vanilla,cardamom and heavy coconut milk(dont add all of it)

4.Acha zichemke kwa dakika 5 
  Let it cooked for 5 minutes 

5.Changanya custard kwenye tui lililobakia na ikoroge vizuri kisha mimina kwenye ndizi baada ya dakika 1 epua
  Mix custard powder and remained coconut milk and pour it in the mixture,leave it for just a minute and remove the pan from the stove

6.Acha zipoe pakua tayari kwa kula kama zilivyo au na wali au na mkate
  Let them cool,serve them as they are or you can serve with bread or rice

Angalizo:Note;
1.Kama ndizi ni ngumu weka tui jepesi jingi ili ziive na zilainike kabla kuweka tui la pili au unaweza kuzichemsha kidogo
 If the plantains are not soft enough better to boil before adding coconut milk .Or add large amount of coconut milk and cook it for a long time before adding the heavy coconut cream

2.Huu upishi haukorogwi so usikoroge hata kidogo tumia kitambaa kisafi cha jikoni kutikisa sufuria
  Do not stir them while cooking.Use the clean kitchen towel and take the pan and shake it if needed 

3.Pika kwa moto wa kiasi kuepusha kuungua
  Cook them by using the middle heat

4.Unaweza kuwekavijiti vinene badala ya maganda ya ndizi ukihofia zitaungua chini
  You can place large stick at the bottom of the pan instead of there skin

5.Zenyewe zina sukari kwahio ukitaka punguza sukari kama hupendi nyingi
  You can reduce the amount of sugar mentioned if you dont like too much sugar

6.Hakikisha tui la mwanzo linakua zito zito ili kupendezesha ndizi zako
  Make sure the first coconut milk is too heavy

7.Hakikisha unaweka maganda au vijiti chini ya sufuria ili zisiungue
  Make sure you place stick or there skin to avoid the plantain to get burnt

Furahia Ndizi Mbivu Zako.

Jumatano, 18 Novemba 2015

TAMBI ZA KUKAANGA



MAHITAJI
1. Tambi Nyembamba Pakti 1
2. Sukari Glasi Ndogo1
3. Hiliki Kiasi
4. Arki Vanilla Kijiko 1
5. Zabibu Kavu Kiasi
6. Mdalasini mzima kiasi   
7. Mafuta Ya Kukaangia Robo Kikombe
8. Maji Glasi Kubwa 2

MAANDALIZI
1.      Pasua tambi zako weka pembeni
2.      Menya hiliki kisha zitwange

JINSI YA KUPIKA
1.Weka mafuta kwenye sufuria anza kukaanga tambi zako mpaka ziwe na rangi ya brown
2. Kisha weka maji,hiliki,sukari,mdalasini,zabibu na arki vanilla
3. Koroga kidogo kuchanganya tambi zako
4. Funika acha zichemke mpaka zikauke
5. Zikikauka funika na mkungu weka mkaa juu yake kama unavyo pika wali acha zikauke vizuri
6. Baada ya dakika 10 epua.
7. Changanya vizuri kisha pakua.


Angalizo: 

1.Ili tambi ziwe nzuri hakikisha maji hayawi mengi ili ziweze kuchambuka.
2.Unaweza kuongeza sukari kama mpenzi wa sukari

Furahia Tambi Zako