Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Mkate. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Mkate. Onyesha machapisho yote

Alhamisi, 3 Novemba 2016

MIKATE YA MAZIWA (MILK BREAD)



MAHITAJI/INGREDIENTS
1.Unga wa Ngano 550gm
  Plain Purpose Flour 550gm

2.Maziwa 300ml
 Milk 300ml

3.Sukari Vijiko 4
 Sugar 4 Tbsp

4.Hamira Vijiko 2
  Yeast 2 Tbsp

5.Chumvi Kijiko Cha Chai 1/2
  Salt 1/2 Tea Spoon

6.Mayai 2
 Eggs 2

7.Maziwa ya Unga Vijiko 2
  Milk Powder 2

8.Ufuta Kijiko 1
  Sesame seeds 1 Tbsp 

9.Siagi Vijiko 2
   Butter 2 Tbsp

10.Unga wa Kusukumia 1/2 Kikombe
   Flour for rolling dough 1/2 Cup

MAANDALIZI/PREPARATIONS
1.Kwenye bakuli changanya unga,maziwa ya unga,sukari,chumvi na hamira
  In a big bowl add flour,milk powder,salt,sugar and yeast 

2.Tumia mwiko kuchanganya vizuri
  Mix all ingredients in a bowl with spartula

3.Ongeza yai moja,siagi na maziwa ya maji
  Add an egg,butter and milk 

4.Kanda unga mpaka uwe mlaini na unavutika
  Mix all and knead the dough till elastick

6.Ufunike uache uumuke vizuri
  Cover the bowl let it rise till double in size

7.Ukisha umuka toa kwenye bakuli ukande kidogo mpaka hewa yote itoke
  Fold the dough until all the air is removed

8.Kata kata donge lako kupata vipande vilivyo sawa na yafanye kuwa maduara
  Spilt the dough into equal pieces and form into round ball

9.Chukua unga mkavu sukuma madonge kwa urefu kisha yazungushe kuanzia ncha ya kwanza hadi ya mwisho
  Use the flour remain and sprinkle to the surface and flatten the balls into long dough then roll it starting from the first end to the last end

10.Rudia kwa madonge yote yalobakia
  Repeat till you finish all balls

11.Paka trei yako mafuta au siagi
  Grease the tray

12.Panga mikate yako
  Keep the bread into the tray 

13.Vunja yai lilobakia na pakaa mikate yako
  Break the egg remain and brush it on the surface of the bread

14.Nyunyizia ufuta mikate yako acha iumuke kwa dakika 20
  Sprinkle the sesame seeds and let them raise for 20 minutes

JINSI YA KUPIKA/HOW TO COOK
1.Washa Jiko la umeme moto wa juu na chini 180'C
  Heat the oven 180'C

2.Oka mikate kwa muda wa dakika 20 mpaka 30
  Bake them for 20 to 30 minutes 

3.Ikiiva itoe jikoni acha ipoe na itoe kwenye trei yake
  When they are ready remove them from the oven let them cool and unmold from the tray

4.Weka kwenye sahani paka siagi tayari kula na kinywaji upendacho 
  Apply butter after that they are ready to serve with any drinks

Angalizo:Note
1.Hakikisha unakanda unga vizuri hadi uwe mlaini
  Make sure you knead the dough till soft

2.Hakikisha mikate inaumuka vizuri kabla kuioka
  The breads must be rise well enough before baking

Furahia Mikate Yako

Ijumaa, 10 Juni 2016

JINSI YA KUPIKA CHAPATI LAINI/HOW TO COOK SOFT CHAPATI


JINSI YA KUPIKA CHAPATI LAINI

MAANDALIZI/PREPARATION
1.Kwanza hakikisha unakanda unga vizuri
 Make sure you knead the dough very well

2.Lazima unga uukande mpaka uwe laini sana
  The kneaded dough must be very soft

3.Baada ya kukata madonge ya idadi ya chapati unazo zitaka
 Divide the dough into any number you want

4.Wakati wa kusukuma tumia unga kuhakikisha unapata duara kubwa kiasi
  Sprinkle the plain flour onto the surface and roll the dough with rolling pin until you get bigger cycle

5.Yeyusha samli au blue band changanya na mafuta kupaka katika duara lako
  Mix the melted butter or ghee with cooking oil and brush on the top of the cycle

6.Kunja unavyopenda ila kumbuka jinsi unavyo ikunja ndio inatengeneza muonekano mzuri wa chapati
  Fold the chapati as you prefer but the chapati good looking depends on how you fold it

7.Baada ya kuziweka mafuta ni vizuri uziache kiasi cha dakika 10 mpaka 15 kabla ya kuzipika 
 After you fold them better to let them rest for atleast 10 to 15 minutes 

8.Sukuma chapati jitahidi upate duara zuri lenye shape ya kuvutia
  Roll the folded dough again to get a nice or perfect circular shape

9.Unapo sukuma chapati isiwe nyembamba wala nene sana iwe na upana wa kiasi
  Make sure it is neither too thin nor too thick

10.Chapati ikiwa nyembamba sana unapo ichoma huwa ina kakamaa na ikiwa nene sana huwa haiivi vizuri inaweza kuwa mbichi
 The thinner dough make chapati to be too crunchy after cooking and the thick chapati can result not to be cooked well inside 

JINSI YA KUPIKA/HOW TO COOK
1.Moto hapa ndio kwenye mambo yote ukikosea chapati nayo inaweza kuwa mbaya
  Heat you use is very important,if you fail to set the required heat and the Chapati will not be good

2.Moto ukiwa mdogo hupelekea chapati kunyonya mafuta
 If you set minimum heat the chapati will absorb oil

3.Moto ukiwa mwingi chapati huungua
 If the heat is high the chapati will be burnt

4.Weka moto wa wastani ili uivishe chapati yako taratibu
 Make sure you set the medium heat during cooking

5.Weka chuma jikoni pakaa mafuta kijiko kimoja
 Heat the pan and add 1 Tbsp of Oil

6.Weka chapati yako jikoni
 Add the Chapati into the pan

7.Iache kidogo sana yaani ikisha kubadilika kutoka ubichi tu geuza upande wa pili
 Leave it for some second before it forms the bubbles flip it to the other side

8.Acha iive mpaka ianze kufanya rangi za kuiva
  Then let the other side cooked evenly till makes golden colour

9.Usiache mpaka ikaungua
 Don't let it burnt

10.Izungushe zungushe kwenye chuma ili sehemu zote zipate ile rangi ya kuiva hasa nchani mwa chapati
 Use your hand to circulate your chapati around the pan so as the corners will cook well

11.Ikunje sehemu mbili sawa
  Fold the Chapati in half

12.Weka mafuta kijiko kimoja
 Add 1 Tbsp of Oil

13.Penyeza kijiko kati kati ya chapati
  Insert the spoon in between of the folded chapati 

14.Fanya kama unaigandamiza huku ukiisugua na chuma
 Press it with spoon around the pan

15.Ongeza mafuta kidogo izungushe chapati hadi upate rangi nzuri ya kuvutia
 Add the little oil and circulate it to get beautiful colour

16.Geuza upande wa pili rudia hatua ya 13 mpaka 16
 Turn the other side of folded chapati and repeat step 13 until 16

17.Ikunjue irudi kuwa duara
 Unfolded the chapati to be in circular shape

18.Acha ule upande wa nyuma ya chapati uive kidogo tu
 Let the white layer to cook evenly

19.Itoe malizia kuchoma chapati zilobakia kwa hatua hizo ziliopo juu
 Remove from the pan and finish the remained chapatis by following above steps

20.Njia hii ya upishi wa chapati hupelekea chapati kuchambuka wakati wa kuipika chapati
 If you cook chapati by this way it makes chapati softer while it is still in a pan 

Angalizo:Note
1.Ukikosea kukanda unga na kuwa mgumu na hizi njia za chini zote zitakataa kutoa chapati laini
 Make sure you knead the dough till soft otherwise the chapati will not be soft

2.Ni vizuri kupika upishi huu ukiwa huna haraka taratibu kupata chapati nzuri
Do not hurry in  preparing and cooking chapati so as to get soft one

3.Ni upishi unaohitaji mazoezi pika mara kwa mara hadi utaziweza
  Make sure you cook chapati frequently so as to get used with it

Furahia Chapati Lainii.

Ijumaa, 22 Aprili 2016

CHAPATI ZA TUI LA NAZI


MAHITAJI
1.Unga wa ngano nusu kilo
2.Tui la nazi ml 500
3.Chumvi kijiko cha chakula 1na nusu
4.Sukari nusu kijiko cha chakula
5.Samli kikombe kidogo cha chai 1
6.Mafuta ya kupikia nusu kikombe

  
MAANDALIZI
1.Chunga unga wako weka kwenye chombo cha kukandia na punguza kikombe kimoja kidogo cha unga mkavu pembeni kwa ajili ya kusukumia
2.Weka chumvi,maziwa,sukari kisha changanya weka pembeni
3.Chukua tui,changanya taratibu mpaka ushikane na kuwa donge
4.Ukande kwa dakika 10 mpaka ulainike
5.Chukua bakuli lenye mfuniko weka donge lako la unga kisha pakaa donge lako lote samli kijiko cha chakula kimoja hakikisha samli inaenea vizuri
6.Funika unga wako kwa dakika 10 kisha utoe endelea kuukanda tena mpaka uwe unavutika kwa dakika 10
7.Katakata madonge kulingana na size ya chapati unayoitaka 
8..Sukuma madonge yako duara kwa kutumia unga mkavu kisha yapake samli kati na sokota na uyapange kwenye bakuli lenye mfuniko na uyaache kwa robo saa
9..Baada ya hapo utaanza kusukuma duara kwa ajili ya kupika chapati


JINSI YA KUPIKA
1.Yeyusha samli ilobaki changanya na mafuta 
2.Weka kikaangio chako jikoni hakikisha moto ni wa wastani
3.Weka chapati yako mpaka ifanye brown
4.Geuza Chapati yako upande wa pili ikiwa ya brown weka mafuta kijiko kimoja
5.Izungushe chapati yako huku ukiikandamiza na kijiko ili kuilainisha kati mpaka nchani 
6.Toa chapati weka nyengine mpaka umalize chapati zako
7.Unaweza kula yenyewe au na maharage,mchuzi,chai,juice,n.k.
8.Hizi chapati zinakuwa laini na ladha nzuri sana.
NB1.Ili chapati ziwe laini hakikisha unakanda kwa muda mrefu mpaka zinalainika
       2.Ipe mda wa kutulia kabla kuipika
       3.Usipende kuiweka mafuta mengi wakati wa kupika
       4.Usigeuze geuze mara kwa mara wakati wa kuchoma
       5.Fanya kama unaivunja vunja ikiwa ya moto kutoka jikoni 

Furahia Chapati Zako.