Jumamosi, 15 Oktoba 2016

UROJO(ZANZIBAR MIX)


Urojo ni mchanganyiko wa vyakula mbali mbali pamoja na uji uji wake katika bakuli moja.
Hapa nitaeleza jinsi ya kuupika huo uji(urojo) mpaka kukamilika kwake.
Asili ya urojo ni India ila kwa sasa nchi mbali mbali zina andaa upishi huu.
Na Zanzibar ni mlo unaopendwa na maarufu sana.Na hii ndio aina ya urojo unaopikwa Zanzibar.

Zanzibar Mix(Urojo) is the dessert prepared by mixing different foods(dessert) with sauce in a bowl.
Its origin is India but now many countries prepared by there own style.
Also in Zanzibar we have our own style on how to prepare Urojo.
I can help you on how to cook this dessert so follow my recipe as follow

Kwenye Urojo Tunaweka/Things added in Mix(Urojo)
1.Mbatata za Kuchemsha
  Boiled Potatoes

2.Mayai Ya Kuchemsha(Ukipenda)
   Boiled Eggs(Optional)

3.Badia

   Badia
 

4.Chatne
  Chatne

5.Chipsi Za Muhogo

   Cassava Chips

6.Mishkaki

  Barbeque

7.Kachori

   Kachori

7.Katlesi(Ukipenda)

   Cutlets(Optional)

8.Na urojo wenyewe

   Urojo Sauce

9.Pilipili(Ukipenda)

  Chilli Sauce(Optional)


Baadhi ya vitu hapo juu nimeshavielezea kwenye blog yangu kwa hio nitaweka links za jinsi ya kuvipika hivyo vitu hapa nitaelezea jinsi ya kupika urojo tu
HIZI NI LINKS ZAKE 

Badia na Chatne(Badia and Chatne) http://mapishiclassic.blogspot.com/2015/11/badia-za-kunde-na-chatne.html


Kachori  http://mapishiclassic.blogspot.com/2016/08/kachori.html

Katlesi(Cutlets) http://mapishiclassic.blogspot.com/2015/11/mahitaji-1.html

Mishkaki(Meat Barbeque) http://mapishiclassic.blogspot.com/2015/12/mishkakibarbeque.html

Chipsi Za Muhogo(Fried Cassava Chips) http://mapishiclassic.blogspot.com/2016/02/chipsi-za-muhogocassava-chips.html

Some of the dessert added in urojo have already explained in my blog on how to prepare them. So I will just keep the links on how to get those recipe.Here I will explain only on how to cook Urojo.
HERE ARE THE LINKS

MAHITAJI/INGREDIENTS

1.Unga wa Ngano Mug 1
  1 Mug Plain Flour

2.Ndimu zilokamuliwa 2
  Lemon Juice(2 Lemon)

3.Maji Lita 2
 2 Litre Water

4.Chumvi Kiasi
 Salt to taste

5.Bizari Kijiko cha chai 1
 1 Tea spoon Turmeric Powder

MAANDALIZI/PREPARATION

1.Weka unga kwenye bakuli kisha weka maji nusu lita pamoja na bizari
   In a bowl add flour,turmeric powder and half liter of water

2.Koroga hadi uhakikishe mabonge yote yameisha
   Stir the mixture until well combined

JINSI YA KUPIKA/HOW TO COOK
1.Mimina maji Yalobakia kwenye sufuria weka chumvi kiasi acha yachemke sana
   Pour the remaining water in the pot with salt and let it boil

2.Kisha mimina uji wenye bizari kwenye maji ya moto taratibu huku ukikoroga mpaka uchanganyike
    Add the turmeric mixture in the boiled and stir it throughly

3.Acha uchemke kidogo kisha mimina ndimu yako na ukoroge kidogo
    Let it boil for a minute than add the lemon juice and stir the mixture

4.Acha uchemke onja chumvi na ndimu kama zipo sawa epua
  Let it boil for some minutes than taste the salt if its okay remove from the heat

5.Ikiwa urojo ni mzito sana ongeza maji acha uchemke kidogo kisha uepue
  If urojo sauce is very heavy  add some water to lighten it

Angalizo:
1.Kama urojo ukiwa mkali au una chumvi nyingi ongeza maji kidogo kidogo mpaka upungue ukali
  Add little water in the sauce if it salty or sour before you remove it from the heat

2.Hakikisha huuachi jikoni kwa muda mrefu mpaka ukaungua
 Make sure you do not let it burnt

3.Usiweke maji mengi ukawa mwepesi kupitiliza
  Do not add too much water the sauce will be too light 

Jinsi ya Kuuandaa/How to serve it



1.Menya Viazi Mbatata ulivyovichemsha kisha vipasue kati na vikate vipande vidogo vidogo
 Take a boiled potatoes and peeled them and cut them into  small pieces

2.Menya Mayai yaliochemshwa na yapasue kati na kata vipande vinne
  Peel the boilede eggs and slice into 4 pieces

3.Chukua Bakuli na kijiko
  Take a bowl and spoon

4.Weka vipande vya viazi ulivyovikata katika kibakuli chenye kijiko
  Add some pieces of boiled potatoes in a bowl having spoon

5.Weka na vipande vya mayai kwenye bakuli
    Add pieces of eggs 

6.Malizia kuweka kachori,badia,mishkaki,chipsi za muhogo na katlesi
   Then add badia,kachori,barbeque,cassava chips and cutlets

7.Kisha mimina urojo kiasi upendacho
   After that pour the urojo sauce in the bowl

8.Weka chatne na pilipili
  Lastly add chatne and chilli sauce

9.Upo tayari kuliwa wenyewe au na mkate upendao na kinywaji upendacho
  Ready to serve with bread,any drinks or as it is

Bakuli lenye urojo kama linavyoonekana
The bowl having Mix(Urojo) as seen after served
Furahia Urojo Wako

0 comments:

Chapisha Maoni