Jumatatu, 4 Aprili 2016

VIAZI MBATATA NA MAYAI(EGG AND ROASTED FRIED POTATOES)



MAHITAJI
  1. Mbatata 8
  2. Nyanya(Tungule) ndogo 2
  3. Chumvi kijiko kidogo 1
  4. Mafuta vijiko vya chakula 4
  5. Tomato paste kijiko cha chakula 1
  6. Yai 1
  7. Kitunguu maji kidogo 1
  8. Royco kijiko 1
  9. Karoti ndogo 1
  10. Pilipili boga(Pilipili hoho) ndogo 1

MAANDALIZI
  1. Osha viungo vyako vyote weka kenye bakuli safi
  2. Menya viazi mbatata na kata kata vipande 4 kwa kila mbatata moja
  3. Kata kata kitunguu maji,keroti na hoho weka pembeni
  4. Para nyanya weka pembeni
  5. Vunja yai weka kwenye kibakuli lipige pige kama unataka kukaanga

JINSI YA KUPIKA
  1. Weka karai la mafuta jikoni acha yapate moto
  2. Weka viazi vyako vikaange mpaka vikaribie kuiva
  3. Weka viazi pembeni kisha kaanga vitunguu mle mle bila kutoa viazi
  4. Kisha weka pilipili hoho endelea kukaanga
  5. Malizia na karoti kaanga zikiwa za brown weka nyanya
  6. Koroga na uweke chumvi na royco kisha funika acha vichemke kwa dakika 1
  7. Weka nyanya ya paketi koroga funika kidogo kwa dakika 1
  8. Mimina yai koroga usiache mkono mpaka livurugike lote lifanye chenga nyeupe
  9. Epua acha ipoe tayari kula na Chapati,mikate yoyote,wali au ugali.

Angalizo:
  1. Usikaange viazi mpaka vikakauka na kuungua
  2. Usiache yai likagandana na viazi
  3. Usiweke maji kwenye upishi huu
  4. Hakikisha unafunika vizuri ukisha kuweka nyanya
  5. Usikaange kwa muda mrefu vitaganda kwenye karai
  6. Unaweza kuweka viungo vya pilau ukipenda pia
  7. Hakikisha tomato paste haiwi nyingi husababisha viazi kuwa vikali


Furahia Viazi Vyako.

0 comments:

Chapisha Maoni