Jumatano, 6 Januari 2016

WALI WA ROSTI(ROASTED RICE)

MAHITAJI
1.Mchele robo
2.Nyama Robo
3.Nyanya(Tungule) kubwa 3
4.Karoti 1
5.Pilipili boga (Pilipili Hoho) 1
9.Kitunguu maji kidogo 1
10.Nyanya pakti vijiko vya chakula 3
11.Vitunguu thomu punje kubwa 3
12.Chumvi kiasi
13.Mafuta vijiko vya chakula 3
14.Tangawizi iliotwangwa kijiko cha chakula 1
15.Viazi mbata vidogo 6
16.Maji kikombe kikubwa cha chai 1

MAANDALIZI
1.Katakata nyama yako na ioshe
2.Chagua mchele na uoshe vizuri
3.Osha viungo vilobakia na viache ndani ya bakuli lenye maji
4.Anza kukata kata vitunguu weka pembeni
5.Katakata pilipili boga weka pembani
6.Kisha katakata karoti kwa urefu nayo iweke pembeni
7.Menya viazi mbatata na weka pembeni


JINSI YAKUPIKA
1.Weka nyama tangawizi na vitunguu thomu vilotwangwa na chumvi jikoni acha kwa dakika 2
2.Weka maji kiasi acha iive
3.Endelea kuweka maji mpaka iive na kuwa laini na iache na supu kidogo sana
4.Weka sufuria nyengine jikoni na weka mafuta
5.Kaanga vitunguu,karoti na pilipili boga
6.Weka viazi viache kwa dakika 1
7.Kisha weka nyanya na chumvi na koroga kisha funika kwa dakika 3
8.Mimina supu yako acha kwa dakika 5 ukiwa umefunika
9.Weka nyanya ya paketi koroga acha kidogo
10.Mimina Maji yaache yachemke vizuri
12.Onja chumvi kama kidogo Ongeza kisha weka mchele wako
13.Koroga kidogo funika mchele wako mpaka maji yakauke
14.Geuza wali wako upambie au ufunike hadi ukauke
15.Ukikauka tayari kwa kuliwa
16.Unaweza kula na salad ama mtupu

Angalizo:
1.Hakikisha unaweka mchele wakati maji yamepungua ili usiwe bwabwa
2.Usikoroge wali mara kwa mara
3.Usiweke maji mengi ukiwa bwabwa haupendezi


Furahia Wali Wako.

0 comments:

Chapisha Maoni