Jumatano, 6 Januari 2016

KEKI YA FRUITS ISIYOKOZA(LIGHT FRUITS CAKE)


MAHITAJI
1.Blue band robo
2.Sukari robo
3.Mayai 6
4.Baking powder kijiko cha chakula 1
5.Unga wa ngano nusu
9.Arki Vanilla kijiko 1
10.Arki ya Ice cream kijiko 1
11.Fruit za keki robo kikombe cha chai
12.Chumvi kiduchu
13.Sukari ya Dandii robo kikombe kidogo cha chai

MAANDALIZI
1.Chunga unga wa ngano weka baking powder na chumvi uchanganye weka pembeni
2.Saga sukari na siagi(Blue band) kwa mkono au hand mixer mpaka ilainike
3.Koroga vizuri kisha weka arki na uchanganye vizuri
4.Vunja mayai weka kwenye mchaganyiko wako wa siagi
5.Weka unga taratibu mpaka mchanganyiko wako uwe uji mzito
6.Weka dandii yako na changanya vizuri mchanganyiko wako
7.Malizia kwa kuweka fruit kisha koroga vizuri
8.Weka kwenye tray au chombo chochote cha kupikia keki

JINSI YAKUPIKA
1.Washa oven kwa moto wa wastani
2.Weka keki yako acha iive mpaka ipige rangi ya brown
3.Chukua kijiti kisafi au tooth pick
4.Chomeka sehemu tofauti kuangalia kama keki imeiva
5.Kijiti kikitoka kikavu keki imeshaiva
6.Kikitika kimaji iache keki ikauke
7.Toa keki ikiiva kata kata tayari kula na Kinywaji upendacho

Angalizo:
1.Hakikisha unaweka moto ambao hauunguzi keki yako
2.Usiweke dandii nyingi keki itakua chungu
3.Usiweke maji
4.Kama unatumia mwiko ni vizuri kutumia mwiko wa ugali kusagia keki yako
5.Hakikisha unaisaga siagi hadi inalainika kama unatumia mkono
6.Unaweza kupika hata kwa mkaa ukikosa oven


Furahia Fruit Cake Yako Zako.

0 comments:

Chapisha Maoni