Jumatano, 6 Januari 2016

VIAZI VITAMU


MAHITAJI
1.Viazi vitamu vikubwa 5
2.Nazi pakti 1
3.Sukari vijiko vha chakula 5
4.Arki Vanilla kijiko cha chai 1
5.Custard kijiko cha chakula 1
9.Hiliki punje 10
10.Chumvi kijiko cha chai 1
11.Maji kiasi

MAANDALIZI
1.Menya viazi na uvikate vipande vidogo vidogo
2.Vioshe na uviweke kwenye sufuria safi na maji kiasi
4.Menya na utwange hiliki
5.Chukua tui gawa sehemu mbili.Robo weka kwenye kikombe lilobakia weka kando
6.Chukua tui robo kikombe weka custard na ikoroge vizuri


JINSI YAKUPIKA
1.Chukua chumvi weka kwenye viazi vyako weka jikoni acha vichemke hadi viive
2.Mwaga maji yaliyobaki acha viazi vilivyo iva bila ya maji
3.Weka tui lililobaki kwenye viazi viloiva pamoja na sukari na hiliki na urudishe jikoni kwa moto wa wastani
4.Acha vichemke kwa dakika 5 hadi tui lipungue
5.Malizia kwa kuweka arki na tui lenye custard
6.Acha dakika 1 jikoni na viepue
7.Acha vipoe pakua tayari kwa kula
8.Inapendeza kula na samaki wa kukaanga

Angalizo:
1.Usiviache vikachemka hadi vikavurugika kabla ya kuweka tui
2.Usikoroge mpaka wakati wa kuvipakua
3.Unaweza kupika na nazi ya kawaida au ya unga
4.Sio lazima kuweka custard


Furahia Viazi Vitamu Vyako.

0 comments:

Chapisha Maoni