Jumatano, 10 Februari 2016

ICE CREAM YA NDIZI (BANANA ICE CREAM)

MAHITAJI
1.Ndizi mbivu 2
2.Maziwa (Whole Milk) nusu lita
3.Sukari vijiko vikubwa 2
4.Arki ya Ice cream kifuniko chake 1
5.Arki Vanilla kifuniko chake 1

MAANDALIZI
1.Menya ndizi weka kwenye jagi la blenda ikiwa imekatwa katwa
2.Mimina maziwa kwenye jagi la blenda
3.Weka sukari na arki zote kwenye jagi

JINSI YA KUTENGEZA
1.Saga mchanganyiko wako mara tatu kila baada ya dakika 1
2.Kisha mimina kwenye chombo chako unachotaka kuweka ice cream yako
3.Weka kwenye friji kwa dakika 20 kisha utoe na usage tena kwa dakika 3
4.Na urudishe kwenye friji kwa masaa mawili
5.Kisha itoe tayari kwa kula
Angalizo
1.Unaweza kutengenezea maziwa yoyote ila whole milk ndio inakupa ice cream laini na nzuri
2.Ukitumia maziwa yenye baridi au barafu hurahisisha kuganda

Furahia Ice Cream Yako.




3 comments:

Unknown alisema ...

arki ndio nini sijaelewa hapo?

Unknown alisema ...

Arki ni Flavor kama Vanilla au Banana na nyenginzo

Unknown alisema ...

I feel the flavour

Chapisha Maoni