Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Keki. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Keki. Onyesha machapisho yote

Jumamosi, 3 Desemba 2016

KEKI RAHISI YA VANILLA NA COCOA(SIMPLE VANILLA AND COCOA CAKE)



MAHITAJI/INGREDIENTS

1.Siagi Robo kilo(1/4 Kg)
  1/4Kg Butter

2.Sukari Robo kilo(1/4 Kg)
 1/4 Kg Sugar

3.Unga Robo kilo(1/4 Kg)
 1/4 Kg Plain Purpose Flour

4.Mayai 6
 6 Eggs

5.Arki Vanilla Kijiko cha chai 1
 1 Tea Spoon Vanilla Essence

6.Cocoa Vijiko vya Chakula 3
 3 Tbsp Cocoa Powder

7.Baking Powder Kijiko Cha Chakula 1
 1 Tbsp Baking Powder

8.Chungwa 1
 1 Orange

7.Maganda ya Chungwa Kijiko Cha Chakula 1
 1 Tbsp Orange Zest

8.Chumvi Kiduchu
 Pinch of Salt

9.Fruit Cake Kikombe Cha Chai Nusu(Sio Lazima)
 1/2 Cup Fruit Cake(Optional)

10.Juisi ya Chungwa Vijiko 3
 3 Tbsp Lemon Juice


MAANDALIZI/PREPARATIONS

1.Chekecha unga kwenye bakuli kisha weka chumvi na baking powder na uchanganye vizuri kwa mwiko
 In a bowl sift the flour then add baking powder and salt,mix them very well by using spartula

2.Osha chungwa vizuri kasha lipare kwa kipario ili upate maganda yake kijiko kimoja
 Wash an orange then grate it till you get one spoon of its zest

3.Weka maganda ya chungwa na Fruit Cake kwenye ungana uchanganye tena vizuri
 Add the orange zest and Fruit Cake in a bowl of flour and mix them very well

4.Weka sukari na siagi kwenye bakuli jengine
  In a separate bowl add sugar and butter

5.Saga mchanganyiko wako kiasi cha dakika 3
 Beat the mixture for atleast 3 minutes

6.Weka Vanilla endelea kusaga kiasi cha dakika 2
 Then add vanilla and keep beating the mixture for 2 minutes

7.Weka mayai yako moja moja mpaka yamalize huku ukiendelea kusaga
 Add the eggs one by one until you complete them alland keep beating the mixture

8.Weka juice ya chungwa kisha saga tena kidogo
 Add lemon juice and keep beating the mixture

9.Malizia kuweka unga kidogo kidogo mpaka umalize wotehuku ukisaga
 Lastly add flour little by little till it finish and beat your mixture

10.Chukua bakuli chota mchanganyiko wako weka miko 3
 In a small bowl add your butter mixture atleast 3 spatula of it

11.Kisha weka cocoa kwenye kibakuli uloweka mchanganyiko wako changanya vizuri kwa kijiko kikubwa
  Add cocoa in that mixture and mix it well by using table spoon

12.Washa Jiko la Umeme moto wa nyuzi joto 160
 Pre heat the oven 160’C

13.Chukua trei weka karatasi ya kupikia
 In a tray add baking paper

14.Kisha Anza kuweka mchanganyiko mweupe na kati weka wa cocoa kasha malizia mweupe
  Start to add white butter mixture and the cocoa mixture at the middle and the white mixture on top

JINSI YA KUPIKA/HOW TO COOK

1.Weka trei jikoni kwa muda wa dakika 50 ndio fungua jiko na tizama keki yako
 Bake the cake for 50 minutes then  open the oven to check it

2.Ingiza kijiti kisafi kwenye sehemu mbali mbali za keki yako kuangalia kama imeiva
 Insert the tooth pick in the cake to check if it is cooked well and done

3.Ikiwa kijiti kitatoka na umaji maji basi keki yako bado rudisha jikoni
 If the tooth pick seems to be wet the cake its not yet cooked return it in the oven

4.Kijiti kikitoka kikavu zima jiko toa keki wacha ipoe
 If the spoon comes dry switch off the oven and remove the cake let it cool

5.Ikipoa toa kwenye trei na ikate vipande tayari kuliwa na kinywaji upendacho
 When it is cool cut it into pieces and serve with any drink you prefer
Angalizo:Note;

1.Hakikisha unafata vipimo sahihi vya unga,siagi,sukari,baking powder na mayai ili upate keki nzuri
  Make sure you use appropriate measurement of butter,sugar,plain purpose flour,baking powder and eggs for best result of the cake

2.Ukikosea vipimo vya keki hupelekea kutoiva au kuwa ngumu
 When the cake ingeredients are misused may not give you soft cake or it may not cooked evenly

3.Kuwa makini na jiko lako kama lina moto mkali tumia nyuzi joto ambazo hazitounguza keki yako
  You know well your Oven so make sure you set appropriate Degrees that may not burn the cake

4.Tumia Chombo ambacho mchanganyiko wa keki hautojaa mpaka juu ili ipate nafasi ya kuiva vizuri kwani ikipata joto hufura na huweza kupelekea mchanganyiko ukamwagika kabla ya kuiva
 Use the tray that has enough space that may not lead the cake mixture to rise and comes out when it is heated

5.Unaweza kupika kwa kutumia mkaa pia
 You can even bake by using charcoal

6.Hakikisha hukati keki yako mpaka ipoe inaweza kupelekea kukatika katika
 Make sure you do not cut your cake if it is not cool enough

7.Keki inaweza kukaa mpaka siku 3 mpaka 4 kwenye mazingira ya joto na siku 6 mpaka 7 kwenye mazingira ya baridi bila kuharibika
 The cake can stay up to 3 to 4 days in hot areas and 6 to 7 days in cold areas

Furahia Keki Yako.



Jumatano, 6 Januari 2016

KEKI YA FRUITS ISIYOKOZA(LIGHT FRUITS CAKE)


MAHITAJI
1.Blue band robo
2.Sukari robo
3.Mayai 6
4.Baking powder kijiko cha chakula 1
5.Unga wa ngano nusu
9.Arki Vanilla kijiko 1
10.Arki ya Ice cream kijiko 1
11.Fruit za keki robo kikombe cha chai
12.Chumvi kiduchu
13.Sukari ya Dandii robo kikombe kidogo cha chai

MAANDALIZI
1.Chunga unga wa ngano weka baking powder na chumvi uchanganye weka pembeni
2.Saga sukari na siagi(Blue band) kwa mkono au hand mixer mpaka ilainike
3.Koroga vizuri kisha weka arki na uchanganye vizuri
4.Vunja mayai weka kwenye mchaganyiko wako wa siagi
5.Weka unga taratibu mpaka mchanganyiko wako uwe uji mzito
6.Weka dandii yako na changanya vizuri mchanganyiko wako
7.Malizia kwa kuweka fruit kisha koroga vizuri
8.Weka kwenye tray au chombo chochote cha kupikia keki

JINSI YAKUPIKA
1.Washa oven kwa moto wa wastani
2.Weka keki yako acha iive mpaka ipige rangi ya brown
3.Chukua kijiti kisafi au tooth pick
4.Chomeka sehemu tofauti kuangalia kama keki imeiva
5.Kijiti kikitoka kikavu keki imeshaiva
6.Kikitika kimaji iache keki ikauke
7.Toa keki ikiiva kata kata tayari kula na Kinywaji upendacho

Angalizo:
1.Hakikisha unaweka moto ambao hauunguzi keki yako
2.Usiweke dandii nyingi keki itakua chungu
3.Usiweke maji
4.Kama unatumia mwiko ni vizuri kutumia mwiko wa ugali kusagia keki yako
5.Hakikisha unaisaga siagi hadi inalainika kama unatumia mkono
6.Unaweza kupika hata kwa mkaa ukikosa oven


Furahia Fruit Cake Yako Zako.